Mapema Jumatatu asubuhi, makamu wa raisi
wa Shirikisho la Soka la Colombia (CONMEBOL) Ramon Jesurun, alikamatwa kwa
mashtaka ya kumpiga mlinzi wa usalama katika mechi hiyo ya fainali. Kulingana
na ripoti, mzozo huo ulitokea mbele ya vyombo vya habari baadae. Jesurun,
pamoja na mtoto wake Ramon Jamil Jesurun, inadaiwa waliagizwa kurudi nyuma na
maafisa wa usalama ambapo wao walikaidi na hatimaye kuingia kwenye mapigano ya
kimwili na mlinzi huyo.
Kukamatwa kwa vigogo hao kunaongeza mzozo
mwingine kwenye fainali ya Copa America ambayo tayari iligubikwa na vurugu za
mashabiki kabla ya mchezo wenyewe. Polisi wa Miami waliwakamata watu kadhaa nje
ya Uwanja wa Hard Rock wakati mashabiki wasio na tiketi wakijaribu kuingia kwa
nguvu uwanjani. Suala la mechi muhimu ya fainali katika mashindano ya Copa
America kugubikwa na vurugu za mashabiki na kukamatwa kwa kiongozi wa juu wa
soka kwa kosa la jinai kunaleta taswira isiyependeza katika mchezo wa soka.
Siku ya kusikilizwa mashtaka ya Jesurun
inatazamiwa kufuatiliwa kwa karibu na jumuiya ya soka ya Colombia na duniani
kote. Tukio hili linaleta maswali kuhusu mwenendo ndani ya vyombo vya uongozi
wa mchezo huu. Je, maafisa wa soka waliokabidhiwa dhamana ya kuongoza
mashirikisho ya soka ni waadilifu kwa kiasi gani?
Usiku wa fainali ya Copa America
ulitakiwa kuwa usiosahaulika katika soka la Amerika Kusini, lakini kwa bahati
mbaya utakumbukwa kwa sababu zisizofaa. Uzuri wa mechi yenyewe ulizuiliwa
na msisimko kutokana na vurugu
zilizotokea nje ya uwanja na kuharibu ladha na sifa za mchezo huu mzuri.

Post a Comment